ITAKUFAIDIA NINI?
Marko 8: 36
Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?
(For what shall it profit a man, if he shall gain the whole world, and lose his own soul?)
▫Itakufaidia nini Kuendelea Kuishi katika Dhambi na Uovu na Kisha kupoteza nafsi yako Kwenye ziwa la moto milele.?
▫Itakufaidia nini kuendelea kuwa rafiki wa dunia na kuwa adui wa Mungu?
▫Itakufaidia nini kumkosa Mungu milele kisa huyo kijana/binti anaye kukosesha ufalme?
▫Itakufaidia nini Kumkosa Mungu kisa dhambi ya Siri unayo endelea kuitenda na hutaki kuchukua Hatua ya kutubu?
▫Itakufaidia nini kuendelea na kazi inayo kufarakanisha na MUNGU na kukosana na MUNGU
▫Itakufaidia
nini kuendelea Kulikosesha kundi la Bwana kwa mafundisho potofu ya
kuwatia moyo kutenda uovu, Huku nafsi zao na mioyo yao inaangamia
dhambini na kukaukiana kila siku?
*Nakupa Shauri Leo ;*
Rejea, Rejea ,
Geuka Geuka,
Ondoka kwenye Comfort zone inayo endelea kutafuna nafsi yako na kuendelea kukauka.
Mdo 3:19 _Tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe , zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana_
✝MAOMBI✝
*Asanthe MUNGU Kwa Neema Yako ya Wokovu. Narejea Kwako. Naomba Neema
Yako Inifundishe Kukataa Ubaya na tamaa za Kidunia na Kuishi maisha ya
haki na utauwa, katika Ulimwengu wa sasa.*
*Kwa Jina la Yesu*
*Ameeen*
🗣Bring
Jesus Christ
To All Nations🌐
No comments:
Post a Comment